Tovuti hii imeanzishwa na Benson Mahenya ili kutoa jukwaa la kupashana habari na kuelimishana miongoni mwa wanamtandao si wa hapa Tanzania tu bali duniani kote. Kwa kuanzia tutatumia lugha za Kiswahili na Kiingereza. Siku za usoni tutaongeza lugha nyingine kama Kifaransa, Kichina, Kitaliano, Kispaniola, Kireno, Kihindi n.k.

Benson Mahenya ni mwanamtandao mahiri ambaye kwa miaka takribani miwili amekuwa akifanya biashara ya mtandao na kampuni moja ya kimataifa inayofanya kazi katika nchi zipatazo 140 na ambayo mauzo yake ya mwaka yapata USD2.5 billion. Baada ya kusoma machapisho mbali mbali na kufundisha watu mikoa mbali mbali nchini Tanzania na nchi za Afrika Mashariki na kusini mwa Afrika kuhusu biashara ya mtandao amegundua ukosefu mkubwa wa vitabu vya Kiswahili kwa wazungumzaji wa lugha ya Kiswahili. Hata wale wanaojua kiingereza hawafanyi jitihada za makusudi za kusoma na kujiendeleza katika fani hii. Ni imani yake kuwa tovuti hiki itawasaidia wasomaji wa lugha ya Kiswahili Afrika Mashariki na duniani kote kuweza kuelewa nini maana ya biashara ya mtandao. Benson anakusudia kufanya kazi kwa karibu na vitivo vya biashara na idara za masoko za vyuo vyote vya elimu ya juu hapa Tanzania, Afrika Mashariki na kwingineko ili kuhakikisha biashara ya mtanda o inapata nafasi stahili katika mitaala ya kozi za masoko na ujasiriamali. Benson alihitimu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kutunukiwa shahada daraja la kwanza katika masuala ya fedha na uongozi (BCom). Benson alishinda skolaship ya Jumuiya ya Madola iliyomuwezesha kwenda Uskochi (Scotland) ambako alisomea shahada ya pili ya masuala ya fedha (MSc) kabla ya kuhitimu tena katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika masuala ya masoko (MBA). Benson pia ni mhitimu wa cheti cha juu cha uhasibu (CPA) na amewahi kufanya kazi katika mashirika mbali mbali ya kimataifa katika sekta ya benki na ukaguzi wa mahesabu kabla ya kuanzisha shughuli zake binafsi za ushauri wa kibiashara na ukaguzi. Benson amesafiri nchi nyingi duniani na anapenda kuwasaidia wajasiriamali wachanga katika biashara zao.
Benson ni mume wa Susan na wana watoto wawili Tusekelege na Gwamaka ambao tayari wanaelewa vilivyo, katika umri wao mdogo, nini biashara ya mtandao!
Facts on Zanzibar
The island is located in the Indian ocean about 35 Km of the coast of mainland Tanzania at six degrees south of equator. Zanzibar is made up of many islands, the main two being Unguja...
Click here for more
Bagamoyo
Bagamoyo is located almost 65 km from the city Centre,Bagamoyo is the most atractive place,our buses will take you there under agreed arangement
Click here for more
Serengeti National park
The Serengeti region encompasses the Serengeti National Park itself, the Ngorongoro Conservation Area,
Click here for more
Ngorongoro Crater
The Ngorongoro Conservation Area or NCA is a conservation area situated 180 km west of Arusha in the Crater Highlands area of Tanzania. The conservation area's boundaries follow the Ngorongoro District. It is 8,288 km˛
Click here for more
Bagamoyo
Bagamoyo is located almost 65 km from the city Centre,Bagamoyo is the most atractive place,our buses will take you there under agreed arangement
Click here for more
Serengeti National park
The Serengeti region encompasses the Serengeti National Park itself, the Ngorongoro Conservation Area,
Click here for more
Welcome to Network Marketing Tanzania- - All rights reserved P.O. Box , Dar Es Salaam , Tanzania -
Mob: +255 716 954 840- Fax: +255 22 2461 066 Email: info@networkmarketingtz.com -
Design by Sam Mujinja E-mail    mujinja@hotmail.com Mob: +255 713 451713,
web counter
Idadi ya Watu
Designed by Sam Mujinja
.